Wataalamu wa wanyamapori Kenya waokoa pundamilia aliyepigwa mshale

Wataalamu wa wanyamapori Kenya waokoa pundamilia aliyepigwa mshale

Pundamilia alitibiwa na wataalamu na akaweza kuinuka na kuendelea na maisha
Pundamilia alikuwa amepigwa Mishale / Picha ya KWS

Huduma ya Wanyamapori ya Kenya, Kenya Wildlife Service inasema wamemuokoa pundamilia alieyekuwa amepigwa mshale.

Wataalamu walimfanyia mnyama huyo oparesheni / picha ya KWS

"Timu ya Huduma ya Wanyamapori ya Kenya (KWS) ikiungwa mkono na Mara North Rangers na Sheldrick Wildlife Trust ilikimbia kumsaidia pundamilia aliyekuwa amepigwa mshale," KWS imesema katika mtandao wa X.

Majeraha ya mshale kwa mnyama huyo yalikuwa makubwa /  picha ya KWS

KWS inasema walimtibu na kumshughulikia kupitia upasuaji papo hapo ili kuchomoa mshale.

"Pundamilia huyu alikuwa na bahati, mshale ulikosa viungo vyake muhimu na haukusababisha madhara makubwa," shirika la Sheldrick Wildlife Trust limesema katika mtandao wake wa X.

Sheldrick Wildlife Trust ni shirika linalohusika katika uokoaji wa wanyama kama tembo na kuhifadhi wanyamapori na maeneo yote ya nyika nchini Kenya.

Pundamilia huyo amerudi kwa mazingira yake / Picha ya KWS

Mshale huo haukuwa umesababisha majeraha makubwa.

Wataalamu hao wanasema mtoto huyo wa pundamilia anatarajiwa kupona kabisa.

Ni muhimu kuzingatia kuwa wanyama wana hatari ya kuwindwa na majangili na wawindaji haramu porini.

TRT Afrika