UNICEF inasema watoto na jamii zilizo katika mazingira hatarishi wako katika hatihati ya kuongezeka kwa mlipuko wa ugonjwa wa MPox / Picha: Reuters

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) siku ya Alhamisi liliomba kiasi cha dola milioni 16.5 ili kuongeza mwitikio wake wa Mpox katika Afrika Mashariki na Kusini.

"Watoto na jamii zilizo katika mazingira hatarishi wako katika hatihati ya kuongezeka kwa mlipuko wa ugonjwa wa Mpox katika eneo hilo kwani kesi zilizothibitishwa zimegunduliwa kote Burundi, Rwanda, Uganda, Kenya na Afrika Kusini," Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mashariki na Kusini mwa Afrika, Etleva Kadilli, amesema katika taarifa.

Burundi hadi sasa imethibitisha zaidi ya maambukizi 500 ya Mpox katika takriban wilaya 25 kati ya 49 za nchi hiyo, kulingana na Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC).

UNICEF imesema watoto na vijana walio chini ya umri wa miaka 20, ni kati ya karibu asilimia 60 ya maambukizi yaliyogunduliwa, na watoto chini ya miaka 5 ni asilimia 21.

"Mbali na mwitikio wa haraka wa kuokoa maisha, juhudi za mawasiliano ya hatari na ushirikiano wa kuvuka mpaka, uwekezaji katika uimarishaji wa mfumo wa afya kwa ujumla, kuendelea kwa huduma muhimu na kuzingatia mipango inayosaidia ustawi wa mtoto kwa ujumla lazima ipewe kipaumbele," alisema Kadilli.

Aina mpya ya virusi vya Mpox (clade Ib) imegunduliwa katika nchi zote zilizoathirika isipokuwa Afrika Kusini, na kuzua wasiwasi kutokana na uwezekano wake wa maambukizi makubwa katika makundi ya umri, hasa watoto wadogo, kulingana na UNICEF.

Pia ilielezea wasiwasi wake kuhusu athari za pili za milipuko ya Mpox kwa watoto na vijana, ikitaja unyanyapaa, ubaguzi na kukatizwa kwa masomo na kujifunza.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inasalia kuwa nchi iliyoathiriwa zaidi na janga hilo, na takriban wagonjwa 18,000 wamerekodiwa tangu mwanzoni mwa 2024, takwimu kutoka Afrika CDC zinaonyesha.

TRT Afrika