| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Rais Ruto ateua wengine wawili katika baraza la mawaziri
Baada ya kuvunja baraza lake la mwaziri Rais William Ruto wa Kenya sasa amependekeza watu 22 kuunda baraza mpya
Rais Ruto ateua wengine wawili katika baraza la mawaziri
Beatrice Askul Moe ameteuliwa katika Wizara ya Masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)/ picha: Wengine / Others
30 Julai 2024

Rais William Ruto amemteua Dorcas Oduor kuwa Mwanasheria Mkuu mpya, Oduor ni wakili wa Mahakama Kuu ya Kenya.

Kwa sasa anahudumu kama Katibu wa Mashtaka ya Umma katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP).

Hapo awali amehudumu katika nyadhifa mbalimbali zikiwemo Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (ODPP), Mkuu wa Idara za Kiuchumi, Kimataifa na Uhalifu (ODPP).

Pia alifanya kazi kama Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na Wakili wa Serikali wa (idara ya Mashtaka ya Umma) katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Wakati huo huo rais Ruto amemteua Beatrice Askul Moe katika Wizara ya Masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Maendeleo ya Kikanda.

Ilikuwa nafasi pekee ambayo ilikuwa bado haijajazwa tangu Rais alipoanza kuunda upya baraza lake la mawaziri.

Moe ni mwanasayansi wa masuala ya kijamii na taaluma mshauri na ujuzi maalumu katika maendeleo na usimamizi wa masuala ya jamii, kuelekea mabadiliko ya kitabia na kijamii katika jamii.

Hadi kuteuliwa kwake, alikuwa mjumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu Uchaguzi ya chama cha ODM, chombo chenye wanachama watatu waliopewa jukumu la kuratibu chaguzi za chama hicho ili kukomesha utamaduni wa kuuza tikiti kwa wazabuni wa juu zaidi.

Aliketi kwenye baraza jipya la uchaguzi na Richard Tairo na Emily Awita kufuatia kuvunjwa kwa Bodi ya Kitaifa ya Uchaguzi.

Hawa wawili watafika mbele ya bunge kwa mahojiano na ukaguzi kabla ya kupitishwa.

Pata habari zaidi kupitia whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika