Kila mpiga kura Rwanda anatakiwa kupiga kura akiwa katika kijiji alichojiandikisha / Picha: Reuters

Raia wa Rwanda watapiga kura Julai 14-16 kumchagua rais na wabunge.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitoa orodha ya mwisho ya wapiga kura Juni 30, ikionyesha kuwa zaidi ya Wanyarwanda milioni 9.5 watashiriki katika uchaguzi huo. Kati ya hao, zaidi ya milioni mbili kati yao watakuwa wapiga kura wa kwanza.

Kila mpiga kura anatakiwa kupiga kura katika kijiji alichojiandikisha.

Tume ya uchaguzi imetoa ruhusa kwa makundi maalumu ya watu kupiga kura katika kituo vyovyote vilivyopo karibu nao, hao ni pamoja na askari wa misheni, waandishi wa habari, wanafunzi wanaofanya mitihani ya kitaifa pamoja na wagonjwa.

Idhini hii pia itapewa wafanyakazi wa dharura, waangalizi wa uchaguzi wa Rwanda, pamoja na wawakilishi wa mashirika ya kisiasa na wagombeaji huru.

Mnamo Julai 14, Wanyarwanda walioko ughaibuni watapiga kura yao. Tarehe 15 Julai, Wanyarwanda nchini humo watampigia kura rais na wabunge.

Tarehe 16 Julai, upigaji kura utafanywa kwa wawakilishi wa makundi maalumu katika Baraza la Manaibu, yaani wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Kuna wagombea watatu wanaowania nafasi ya Urais: Paul Kagame wa RPF-Inkotanyi na vyama washirika wake, Frank Habineza wa Democratic Green Party, na Philippe Mpayimana mgombea binafsi.

TRT Afrika