Watu watatu wamekufa katika maporomoko mapya ya ardhi Kusini mwa Ethiopia / Photo: AFP

Maporomoko ya ardhi yaliyosababishwa na mvua kubwa katika Wilaya ya Decha, Kanda ya Kafa, nchini Ethiopia yamesababisha vifo vya watu watatu na kuwahamisha wakazi 24, kulingana na Ofisi ya Mawasiliano ya Kanda ya Kafa.

Maafa hayo yalitokea Julai 25, 2024.

Watu watatu waliofariki walikuwa wa familia moja, na mtu mmoja pia alijeruhiwa katika tukio hilo. Ofisi ya mawasiliano iliendelea kusema kuwa familia zilizoathiriwa zimehamishwa hadi kwenye vituo vya serikali huko Kebele kutokana na hatari kubwa ya maporomoko zaidi na kuathirika kwa nyumba nyingi katika eneo hilo.

Maporomoko haya ya ardhi huko Kafa yanakuja baada ya maporomoko mabaya ya ardhi katika kijiji cha Kencho Shacha Gozdi, Kanda ya Gofa, Jimbo la Kusini mwa Ethiopia, na kusababisha zaidi ya watu 257 kupoteza maisha.

Maporomoko mengine yaliwauwa watu 260 katika kijiji cha Kencho Shacha Gozdi, Kanda ya Gofa, Jimbo la Kusini mwa Ethiopia 23 Julai 2024/ Picha: Reuters 

Kwa mujibu wa Tume ya Kudhibiti Hatari nchini humo, takriban watu 6,000 walio katika mazingira magumu wametambuliwa kuhamishwa kutoka eneo la maafa wakiwemo watu 600, ambao tayari wamehamishwa kutoka eneo hilo.

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) iliripoti kwamba maafisa wa eneo hilo wanatarajia idadi ya vifo kuongezeka hadi watu 500.

OCHA inakadiria kuwa zaidi ya watu 15,000, ikiwa ni pamoja na watoto 1,320 chini ya miaka 5 na 5,293 wajawazito na wanaonyonyesha, wako katika hatari kubwa na wanahitaji kuhamishwa mara moja.

Serikali inaendelea na mpango wa uokoaji kwa ushirikiano na mamlaka za kikanda na kanda.

TRT Afrika