Toleo la mwisho la 2022 lilikuwa na zaidi ya nchi 20 zilizoshiriki./ Picha: ADD (toleo la 2022)

Anga juu ya Kituo cha Jeshi la Anga cha Waterkloof huko Centurion, Pretoria, Afrika Kusini, kuanzia Jumatano, Septemba 18, itakuwa na msururu wa sarakasi za angani za kustaajabisha, ndege za kijeshi, na maonyesho ya ajabu ya anga.

Hii ni wakati toleo la 12 la maonyesho ya Anga ya anga na Ulinzi ya Afrika (AAD) yanapoanza kwa maonyesho ya ndege za kisasa, ndege zisizo na rubani na vifaa vya ulinzi.

Tukio hilo linaonyesha ndege na vifaa vya kijeshi. / Picha: ADD (Toleo la 2022)

Tukio hilo, ambalo litaendelea hadi tarehe 22 Septemba, limeandaliwa ili kuonyesha ndege za kijeshi za ulinzi kutoka kwa makampuni makubwa ya anga na ulinzi katika bara la Afrika na kwingineko.

Kampuni za kijeshi kutoka Kenya, Afrika Kusini, Botswana, Senegal, na Morocco zitaungana na wenzao kutoka nje ya bara hilo kuonyesha umahiri wao.

Waandalizi wanasema onyesho hilo litainua uchumi wa Afrika Kusini. /Picha: ADD (Toleo la 2022)

"Toleo hili la 12 la AAD halingeweza kuja kwa wakati mzuri zaidi, kwani linalingana na miaka 30 ya demokrasia ya Afrika Kusini. Pia inasisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na serikali,” Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya AAD, Bi. Segomotso Tire, alisema katika taarifa yake.

Onyesho hilo huwasaidia vijana wanaojifunza kutafuta fursa katika sayansi na teknolojia. / Picha: ADD (Toleo la 2022)

Waandalizi wanasema onyesho hilo pia litakuwa na Mpango wa Maendeleo ya Vijana (YDP) ambao huleta pamoja maelfu ya wanafunzi chipukizi kutafuta fursa za sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati.

Hafla hiyo hufanyika kila mwaka nchini Afrika Kusini, huku waandaaji wakisema "imechukua jukumu muhimu katika kukuza uchumi wa Afrika Kusini kwa kupata mapato makubwa kupitia mauzo ya tikiti, ukarimu, na utalii na kuunda kazi nyingi."

Onyesho la anga lina maonyesho ya kusisimua. /Picha: ADD (Toleo la 2022)

Mnamo mwaka wa 2022, maonyesho hayo yalitoa zaidi ya nafasi za kazi 1,350, huku wageni wa kimataifa wakichangia zaidi ya randi milioni 135 ($7,678,373) kwa Pato la Taifa (GDP).

Onyesho hilo linatarajia kukuza ushirikiano wa kimataifa. / Picha: ADD

Kulingana na waangaji, walisisitiza ya kwamba, kipengele kingine cha nguvu zaidi cha hafla hiyo, hata hivyo, ni kukuza ushirikiano wa kimataifa na ushirikiano kati ya tasnia ya ulinzi na serikali.

TRT Afrika