Wananchi Nairobi waandamana mbele ya mkutano wa kutafuta sheria za kupunguza uchafuzi wa plastiki  / Picha AFP

Mkutano wa kimataifa wa kujadili swala la plastiki ambao utafanyika Nairobi wiki ijayo una nia ya kuunda sera ya kimataifa juu ya uchafuzi wa plastiki, pamoja na mazingira ya baharini.

Waandamanaji wanataka kuwe na sheria ya kimataifa kupunguza uchafuzi wa plastiki/ Picha AFP 

Umoja wa matifa unaonya kuwa bila hatua za haraka, takriban tani milioni 11 za plastiki zinazoingia baharini kwa mwaka zitaongezeka mara tatu katika miaka ishirini ijayo.

Hii itamaanisha kati ya tani milioni 23 na 37 za plastiki zitatiririka baharini kila mwaka ifikapo mwaka wa 2040.

Sheria muafaka zisipowekwa kuhusu plastiki UN inaonya kuwa kutakuwana ongezeko ya uchafuzi wa plastiki ardhini na majini/ Reuters 

Wataalamu wanasema kuwa kuchakata tena hakuwezi kumaliza uchafuzi wa plastiki na kwamba ubinadamu unahitaji kutumika na kutoa nyenzo kidogo.

UN inaonya kuwa kuna ongezeako ya uchafuzi wa plastiki duniani / Picha: AFP 

UN inasema kuwa zaidi ya tani bilioni 6.5 ya platiki inazunguka duniani na uchafuzi wa plastiki umepatikana katika kila mfumo wa ikolojia, ardhini na majini.

Inaongezea kuwa chembe ndogo ndogo za plastiki pia zimeripotiwa kupatikana katika sehemu ya miili ya binadamu, kwenye damu, na maziwa ya mama, na kusababisha vitisho kwa afya ya binadamu kutokana na viungio vya sumu katika bidhaa za plastiki.

Plastiki zina athari kwa ardhi na hata majini / Picha : AFP 

Nchi 34 kati ya 54 barani Afrika zimepitisha sheria ya kupiga marufuku plastiki na kuitekeleza au kupitisha sheria kwa nia ya utekelezaji.

Nchi 34 barani Afrika zimepitisha sheria dhidi ya plastiki lakini utimizaji kwa nyingi ni changamoto / picha: AFP 

Kati ya hizo, 16 wamepiga marufuku kabisa mifuko ya plastiki au wamefanya hivyo kwa sehemu kadhaa lakini chnagmpoto ni kuwa bado nyingi hazijawasilisha sheria za kutekeleza marufuku hiyo.

TRT Afrika