Maoni ya Tyla yalizua hisia tofauti mtandaoni. /Picha: Picha za Getty

Mwimbaji wa Afrika Kusini Tyla alitoa kauli nzito katika Tuzo za Muziki za MTV za mwaka wa 2024 alipopokea Tuzo Bora ya Afrobeats kwa wimbo wake wa "Water."

Katika hotuba yake , Tyla alisisitiza utofauti wa muziki wa Kiafrika, akitoa wito wa kutambulika zaidi kwa muziki tofauti na ule wa 'Afrobeats'.

"Najua kuna tabia ya kuwaweka wasanii wote wa Afrika katika kundi la Afrobeats. Ingawa Afrobeats imeendesha mambo na kufungua milango kwetu, muziki wa Kiafrika ni wa aina mbalimbali.

"Mimi natoka Afrika Kusini, nawakilisha 'Amapiano' na utamaduni wangu," alisisitiza Tyla.

Maoni yake yalizua mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii, huku wengi wakimpongeza kwa kuangazia umuhimu wa kutambua urithi wa muziki wa Afrika.

Utofauti wa muziki wa Kiafrika

Baadhi ya waangalizi walidai kuwa Afrika inastahili kategoria nyingi ili kuonyesha sauti zake tofauti.

"Kwa maneno mengine, Afrika inahitaji zaidi ya aina moja. Ndiyo! Ni sawa. Amapiano ni utamaduni wetu wa muziki wa Afrika Kusini, kusema ukweli. Tanzania ina wenyewe, hivyo hivyo na Ghana,” shabiki mmoja aliandika kwenye mtandao wa X.

Hata hivyo, matamshi ya Tyla pia yalileta ukosoaji kutoka kwa baadhi ya watu, akiwemo mwanahabari Do2tun, ambaye alitilia shaka uamuzi wake wa kukubali tuzo hiyo ikiwa anahisi haikumwakilisha.

"Ikiwa ulifikiri kuwa umeainishwa katika kategoria isiyofaa, unapaswa kurudisha tuzo au kukataa uteuzi. Ulichukua kwa uwazi tuzo ambayo haikuwakilisha," Do2tun alisema kwenye akaunti yake ya Instagram.

Kutozingatiwa Afrobreats pekee

Matamshi ya Tyla yanaonyesha mwelekeo unaokua miongoni mwa wasanii wadogo wa Kiafrika ambao wanajitenga na aina ya Afrobeats.

Wasanii kama Burna Boy, Rema, na Fireboy DML wamekubali utambulisho mpya wa muziki, wakigundua sauti zaidi ya mfumo wa kitamaduni wa Afrobeats.

Ingawa Afrobeats bila shaka imekuwa na jukumu kubwa katika kueneza muziki wa Kiafrika kimataifa, nyota hawa wanasema ni muhimu kutambua utofauti mkubwa wa muziki wa bara hilo.

Katika usiku wa tuzo za MTV, mashabiki wanamsifu Tyla kwa kufanikiwa kusaidia kupinga kuzingatiwa zaidi kwa Afrobeats na badala yake kuzingatiwa kwa kwa aina zingine nyingi za muziki ambazo Afrika inapaswa kutoa.

TRT Afrika