Deby Itno ashinda uchaguzi wa urais nchini Chad. / Picha: AFP

Rais wa Mpito wa Chad Mahamat Idriss Deby Itno ametangazwa mshindi wa uchaguzi wa urais, kulingana na matokeo ya mwanzo.

Shirika la kitaifa linalosimamia uchaguzi wa Chad lilitoa matokeo ya uchaguzi jioni ya siku ya Alhamisi, 9 Mei, wiki moja mapema kuliko ilivyopangwa. Takwimu hizo zilionyesha Deby Itno alishinda kwa zaidi ya asilimia 61 ya kura, huku mshindi wa pili Succes Masra akiwa nyuma kwa zaidi ya asilimia 18.5 ya kura.

Chad ilifanya uchaguzi wake wa urais uliochelewa kwa muda mrefu siku ya Jumatatu kufuatia miezi 24 ya awamu ya mpito wa kijeshi ulioamuliwa tarehe 1 Oktoba 2022. Uamuzi huo ulifungua njia kwa Baraza la Mpito la Kijeshi na Rais Mahamat Idriss Deby Itno kuendelea na uongozi wake. Pia uliamua rais na wajumbe wa Baraza la Mpito la Kijeshi kuwa wagombea katika uchaguzi unaokuja.

Nchi inayouza mafuta yenye takriban watu milioni 18 ilipata uhuru mwaka 1960 baada ya miongo kadhaa ya utawala wa kikoloni wa Ufaransa.

Moja ya nchi zenye maendeleo duni duniani, rasilimali zilizo chache za Chad zimezidi kupungua kutokana na misukosuko mingi, ikiwa ni pamoja na mawimbi ya joto yanayochochewa na hali ya hewa na mzozo wa wakimbizi unaohusishwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe katika nchi jirani ya Sudan.

TRT World