Matia Kasaija, Uganda Minister of Finance, Planning & Economic Development, Republic of Uganda photo by Parliament of Uganda

Waziri wa Fedha wa Uganda Matia Kasaija alisoma bajeti ya nchi hiyo ya Mwaka 2024/2025 ambayo ilionyesha lengo la serikali kutumia Shs72.1trillion kwa mwaka huu wa kifedha.

Waziri Kasaija alisema kuwa hadi kufikia mwishoni mwa Disemba 2023, jumla ya deni la umma la Uganda lilifikia dola bilioni 25.2 (Ush93.38 trilioni). Kati ya fedha hizo, deni la nje lilikuwa dola bilioni14.9 (USh55.37 trilioni) wakati deni la ndani lilikuwa dola bilioni10.2 (USh38.01 trilioni).

"Bajeti hii kwa kiasi kikubwa kwa wananchi ambao bado wamekwama katika uchumi wa kujikimu," Kasaija alisema wakati akiwasilisha bajeti.

Uganda imeondowa ushuru kwa wawekezaji katika mauzo ya hisa katika hisa kibinafsi au fedha za mtaji zinazodhibitiwa na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji. Nia ni kuhamasisha usawa kibinafsi au uwekezaji wa mtaji wa mradi nchini Uganda.

Uganda imeongeza ushuru kwa petroli na dizeli/ picha: AP

Uganda imeondoa ushuru kwa muda wa mapato ya mtu anayetengeneza magari ya umeme, pikipiki za umeme, betri za umeme na vifaa vya kuchaji magari ya umeme.

Mtu anayeunda, kuanzisha au kuendesha kituo cha matibabu au kituo cha matibabu au hospitali atapata likizo ya ushuru.

Dola milioni 77 (Ugshs bilioni 289.6) zimetolewa kwa ajili ya kuendeleza utalii, ikisema utalii una faida kubwa kwenye uwekezaji.

Pia Uganda imeanza kutoza ushuru wa zuio wa asilimia 10 kwenye kamisheni inayolipwa kwa mawakala wa benki na mawakala wa fintech (watoa huduma za malipo).

Ushuru mpya

Ushuru umewekwa kwa bidhaa tofauti:

i) Ushuru wa Bidhaa kwenye bia ya unga kwa Sh 1,000 kwa kilo.

ii) Ushuru wa Bidhaa kwa kiwango cha asilimia 0.5 ya thamani ya kupokea fedha kutoka kwenye majukwaa mengine tofauti na huduma za makampuni ya simu. Hii haihusishi mtu kupokea pesa kupitia kwa wakala wa benki au benki.

Wawekezaji kwa kituo cha hospitali au kituo cha matibabu watapata likizo ya ushuru/ picha: Hospitali ya Mulago

Ongezeko la Ushuru

Seriklai imependekeza ongezeko la ushuru wa bidhaa kwa:

1) Petroli kwa Sh 100 kwa lita

ii) Dizeli kwa Sh.100 kwa lita.

iii) Mvinyo unaoagizwa kutoka nje ya nchi kutoka asilimia 80 au dola 2.15

(Ugsh 8,000) kwa lita hadi asilimia 100 au dola 2.7 (Sh 10,000) kutegemea ipi ni kubwa zaidi.

vi). Viambatisho, viungio, simenti nyeupe na chokaa. Lengo ni kuoanisha ushuru wa bidhaa hizi na ule wa saruji.

Katika mwaka wa fedha wa 2023/24, Serikali ilisaidia kaya 53,930 kwa chakula cha msaada na bidhaa zisizo za chakula kote nchini.

Mwaka ujao wa fedha, waziri ametoa Shilingi bilioni 18.1 pamoja na Mfuko wa Dharura wa dola milioni 39.3 (Ugsh bilioni 146.26) kusaidia kukabiliana na maafa, ikiwa ni pamoja na:

i. Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kudhibiti Hatari za Maafa.

ii. Kusaidia kaya 50,000 kwa chakula na bidhaa zisizo za chakula kote nchini.

iii. Utoaji wa fedha kwa Uganda Red Cross kusaidia walioathiriwa na maafa.

Sekta ya sheria imewekewa jumla ya dola bilioni 2.6 (Ugsh trilioni 9.588).

Dola milioni 247.9 (Ugsh bilioni 920.86) imetengwa kwa ajili ya sekta ya mafuta na gesi/Picha :TRT Afrika

Kati ya hizo dola milioni 126.9 (Ugsh bilioni 481.4) ni kwa ajili ya usimamizi wa haki, serikali ikisema hii ni kwa ajili ya kuhakikisha kuwa Uganda inabaki kuwa nchi yenye amani na uwajibikaji na wananchi watiifu wa sheria.

Katika mwaka ujao wa fedha, Waziri ametangaza dola milioni 264 (Ugsh bilioni 982.56) kwa ajili ya kuongezeka kwa upatikanaji wa umeme kupitia miradi ya upanuzi na uunganishaji wa gridi ya taifa.

Hii pia inatarajiwa kusaidia uwekezaji zaidi katika ujenzi wa mitandao ya usafirishaji na usambazaji umeme unaolenga vituo vya mizigo ili kukuza uongezaji thamani.

Dola bilioni 1.34 (Ugsh4.989 trillioni) zimetengwa kwa ajili ya ujenzi na urekebishaji wa mabarabara tofauti nchini.

Mwaka ujao wa fedha serikali hiyo imetenga dola milioni 247.9 (Ugsh bilioni 920.86) kwa ajili ya sekta ya mafuta na gesi. Hii inalenga uendelezaji wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) mjini Tanga.

Pia inalenga kuendelea kwa ujenzi wa EACOP ikiwa ni pamoja na miundombinu muhimu ili kuwezesha uzingatiaji wa viwango vya juu vya mazingira.

TRT Afrika