Reli hii itarekebishwa kupitia mkataba wa miaka 30 na wawekezaji / Picha: Reuters kumbukumbu  / Photo: Reuters Archive

Angola na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zinatumai mradi wa kurekebisha reli ya kitambo inayounganisha maeneo ya bara yenye madini mengi na bahari ya Atlantiki utasaidia katika kufufua uchumi.

Luanda na Kinshasa zilitoa mkataba wa miaka 30 kwa wawekezaji, wiki iliyopita ili kuboresha barabara hii ya reli inayounganisha bandari ya Angola ya Lobito na Kolwezi, mji wa kusini katikati mwa ukanda wa shaba wa DRC.

Mradi huo unatarajiwa kuanza baada ya miezi mitatu.

Wachambuzi wanasema mradi huo wenye thamani ya dola milioni 555, unaofadhiliwa kwa kiasi na Marekani, unatarajiwa kuongeza mauzo ya nje ya madini na biashara ya ndani ya Afrika.

"Kufungua ukanda wa Lobito... ni eneo la kihistoria," Alex Vines alisema katika majadiliano yaliyofanyika katika makao ya shirika la Uingereza Chatham House.

Kwa sasa ikiwa na urefu wa kilomita 1,700 reli hiyo ilikamilishwa karibu miaka 100 iliyopita na wawekezaji wa Uingereza waliokuwa na nia ya kupata shaba kutoka Afrika.

Upande wa reli nchini Angola ilifungwa wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya 1975 na 2002 nchini humo.

Ilibaki bila kutumika baadaye kwa sababu ya uharibifu. Ilijengwa upya na kampuni ya Uchina, ikafunguliwa tena mnamo 2015 lakini usafiri umekuwa mdogo.

Barabara mpya

" Eneo la Kongo lilianza nyakati za ukoloni na halitunzwi vizuri," alisema Marcel Lungange, mkuu wa miundombinu katika kampuni ya kitaifa ya reli ya DRC, SNCC.

“Tuna uwezekano wa reli kuharibika mara tatu kwa siku kutokana na uchakavu wa njia za reli, huku treni zetu zikiwa na kasi ya kilomita mbili kwa saa katika maeneo mengi,” alisema.

Makampuni ya uchimbaji madini mara nyingi yanasafirisha madini kutumia malori kwenda katika bandari zenye msongamano mara nyingi nchini Tanzania, Msumbiji na Afrika Kusini. Lakini safari kama hizo ni ghali na huchukua wiki kukamilika.

Wakala wa Kimataifa wa Nishati, yaani International Energy Agency, unatarajia mahitaji ya kimataifa ya madini muhimu kuongezeka mara nne ifikapo mwaka 2040.

Haya yanajiri wakati nchi zikikimbia kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa, njia mpya za usafirishaji nje zinahitajika sana, alisema Louis Watum, ambaye anaongoza Chama cha Wachimbaji Madini cha DRC, kikundi cha wafanyabiashara.

Uunganisho wa Zambia

DRC ndiyo mzalishaji mkuu zaidi wa dunia na barani Afrika wa kobalti na shaba. Madini yote mawili hutumiwa kujenga paneli za kunasa miale ya jua, mashamba ya upepo na magari ya umeme.

"Tayari tuna foleni kubwa za malori" kwenye vituo vya mpaka, Watum alisema.

Muungano huo, unaojumuisha mfanyabiashara wa kimataifa wa Trafigura na kampuni ya ujenzi ya Ureno ya Mota-Engil, unatumai reli iliyoboreshwa itapunguza muda wa usafiri kutoka DRC hadi Lobito hadi chini ya saa 36.

Inataka kuwa na angalau treni sita kwa siku zinazovuka ndani na nje ya nchi ndani ya miaka mitano.

Kwa maana hiyo inapanga kuwekeza dola milioni 455 katika uboreshaji nchini Angola, ikiwa ni pamoja na kununua zaidi ya mabehewa mapya 1,500 ya treni, kuimarisha madaraja na reli za kuchomelea.

Dola nyingine milioni 100 zimetengwa kwa ajili ya DRC, huku makubaliano ya mkataba yanalenga pia kupanua njia hadi nchi jirani ya Zambia.

Takriban nusu ya fedha hizo zinatarajiwa kufadhiliwa na Shirika la Maendeleo na fedha la Marekani, US International Development Finance Corporation.

Makampuni ya uchimbaji madini yanapendelea kusafirisha metali kupitia lori hadi bandari zenye msongamano mara nyingi nchini Tanzania, Msumbiji na Afrika Kusini -- lakini safari kama hizo ni ghali na huchukua wiki kukamilika. Huku Wakala wa Kimataifa wa Nishati ukitarajia mahitaji ya kimataifa ya metali muhimu kuongezeka mara nne ifikapo mwaka 2040 wakati nchi zikikimbia kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa, njia mpya za usafirishaji nje zinahitajika sana, alisema Louis Watum, ambaye anaongoza Chama cha Wachimbaji Madini cha DRC, kikundi cha wafanyabiashara.

TRT Afrika