Ajali ya basi Uganda yaua watu 8 na kuwajeruhi wengine 37

Ajali ya basi Uganda yaua watu 8 na kuwajeruhi wengine 37

Ajali ya basi katikati mwa Uganda imeua takriban watu 8 na wengine 37 kujeruhiwa.
Basi hilo liligongana uso kwa uso na lori katikati mwa Uganda mnamo Agosti 19,2024. /Picha: Reuters

Takriban watu 8 waliuawa na wengine 37 kujeruhiwa katika ajali ya mgongano wa uso kwa uso kati ya basi na lori katikati mwa Uganda Jumatatu.

Ajali hiyo ilitokea wakati dereva wa basi hilo, anayeripotiwa kuwa mwendo kasi na kujaribu kulipita gari lingine, alishindwa kulidhibiti gari hilo.

Basi hilo liligongana uso kwa uso na lori lililokuwa limepakia unga wa mahindi.

Polisi wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwa sasa wanaendelea na uchunguzi.

Kamanda wa Polisi mkoani humo Twaha Kasirye alitaja ajali hiyo kuwa ni mwendo kasi na kubainisha kuwa dereva alikuwa akiharakisha kutimiza ratiba yake jijini Kampala.

Uganda imepata ongezeko la asilimia 30% la vifo vya barabarani katika mwaka uliopita, huku vifo 4,179 vimerekodiwa, kulingana na ripoti ya hivi punde ya trafiki na usalama.

Hatua mpya za usalama barabarani

Katika kukabiliana na ongezeko la idadi ya ajali, serikali ya Uganda imeanzisha hatua mpya za usalama barabarani.

Hatua hizi ni pamoja na ongezeko mara kumi la faini za mwendokasi, kutoka dola 55 hadi dola 550 za Marekani, kama sehemu ya Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Trafiki na Usalama Barabarani wa 2023.

Kiwango cha juu cha mwendo kasi katika barabara kuu sasa kimewekwa kuwa kilomita 100 kwa saa, na kilomita 80 kwa saa kwenye barabara za lami au changarawe.

TRT Afrika