| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo.
Emine Erdogan amesema kuwa mazungumzo yao yalilenga masuala ya mshikamano wa kijamii yanayohusu ubinadamu kwa ujumla, huku akieleza matumaini kwamba ziara hiyo itaimarisha uhusiano wa nchi hizo mbili katika nyanja zote.
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo.
Wake wa marais hao wamekutana katika Ikulu ya Al-Ittihadiya, walijadili masuala yaliyolenga mshikamano wa kijamii. / Wengine / Others
tokea masaa 3

Mke wa Rais wa Uturuki, Emine Erdogan, amekutana na Mke wa Rais wa Misri, Entissar Amer, katika mji mkuu wa Misri Cairo, kama sehemu ya ziara rasmi ya Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan nchini Misri.

Mkutano huo ulifanyika siku ya Jumatano katika Ikulu ya Al-Ittihadiya, ambapo wake hao wa marais walifanya mazungumzo yaliyolenga masuala ya mshikamano wa kijamii, kulingana na taarifa iliyowekwa na Emine Erdogan.

“Tulifanya mkutano wenye manufaa kuhusu masuala ya mshikamano wa kijamii yanayogusa kwa karibu ubinadamu kwa ujumla,” Mke wa Rais Erdogan aliandika kupitia jukwaa la kijamii la Uturuki, NSosyal.

Baada ya mazungumzo hayo, wake hao wa marais walitembelea Jumba la Makumbusho ya Misri (Grand Egyptian Museum), yenye zaidi ya mabaki ya kihistoria 57,000 yanayoonyesha historia ya Misri, kisha wakatembelea ‘piramidi’ katika eneo la Giza.

Akizungumzia ziara hiyo, Emine Erdogan alisema kuwa mapiramidi, katika jangwa, yanaashiria uhusiano wenye nguvu kati ya siku zamani na siku zijazo, na yana nafasi ya kipekee katika kumbukumbu ya pamoja ya wanadamu.

Alisema alifurahi kuona Piramidi Kuu ya Khufu, mojawapo ya Maajabu Saba ya Dunia ya Kale, ana kwa ana.

“Natumaini ziara hii yenye thamani itachangia kuimarika kwa uhusiano kati ya nchi zetu katika nyanja zote,” alisisitiza.

Hapo awali, Rais Erdogan alipokelewa jijini Cairo na Rais wa Misri, Abdel Fattah el-Sisi.

Rais Erdogan ameandamana katika ziara hiyo na maafisa wengi waandamizi wa Uturuki, wakiwemo mawaziri muhimu.

Wakati wa ziara hiyo, mikataba mingi katika sekta mbalimbali pia imesainiwa na taasisi na wizara husika za nchi hizo mbili.

CHANZO:TRT World and Agencies