| Swahili
UTURUKI
2 DK KUSOMA
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na wa Jordan wajadili suala la Gaza, Syria
Hakan Fidan na Ayman Safadi wamejadiliana mahusiano ya nchi mbili pamoja na masuala ya kikanda.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na wa Jordan wajadili suala la Gaza, Syria
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan./Picha: AA / Others
27 Januari 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan na mwenzake kutoka Jordan Ayman Safadi wamekuwa na mazungumzo ya simu, wakijadiliana kuhusu hali halisi inayoendelea Syria na Gaza, kulingana na vyanzo vya kidiplomasia vya Uturuki.

Wawili hao, pia walipata fursa ya kujadiliana uhusiano wa nchi hizo mbili pamoja na masuala ya kikanda, siku ya Jumatatu.

Safadi aliitembelea Ankara mnamo tarehe 6 Januari na kuwa na mkutano wa pamoja na wanahabari akiwa na Fidan.

Safadi aligusia umuhimu wa kukuza ushirikiano na uratibu kati ya nchi hizo wakati wa mkutano huo ili kuweza kutatua changamoto za kikanda, ikiwemo mchakato wa ujenzi mpya wa Syria na urejeshwaji wa utulivu katika eneo la Mashariki ya Kati.

Safadi pia alikazia jitihada za Jordan kuunga mkono watu wa Palestina katika mapambano yao ya kuwa na dola yao huru kwa kuzingatia mipaka ya 1967.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika