Uturuki inatoa wito kwa jumuiya nzima ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti kukomesha ukatili wa Israel huko Gaza na kulitambua taifa la Palestina. / Picha: TRT World  

Uturuki imeunga mkono azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linalopanua haki na hadhi ya Palestina katika Umoja wa Mataifa.

"Azimio hili linathibitisha uungaji mkono mkubwa wa jumuiya ya kimataifa kwa haki ya watu wa Palestina ya taifa lao wenyewe na suluhisho la serikali mbili," Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki ilisema katika taarifa yake siku ya Ijumaa.

Kwa kuzingatia azimio hilo, Uturuki inatoa wito kwa jumuiya nzima ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti kukomesha ukatili wa Israel huko Gaza na kulitambua taifa la Palestina.

Awali Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipiga kura kwa kiasi kikubwa kutoa "haki na hadhi " mpya kwa Palestina na kutoa wito kwa Baraza la Usalama kufikiria upya ombi lake la kuwa mwanachama wa 194 wa Umoja wa Mataifa.

Baraza hilo la wanachama 193 duniani liliidhinisha azimio hilo lililofadhiliwa na Waarabu na Wapalestina kwa kura 143-9 huku 25 zikipiga kura siku ya Ijumaa.

'Mazungumzo na Israeli'

Marekani ilipinga azimio la baraza lililoungwa mkono na watu wengi mnamo Aprili 18 ambalo lingefungua njia ya uanachama kamili wa Umoja wa Mataifa kwa Palestina, lengo ambalo Wapalestina wamekuwa wakitafuta kwa muda mrefu huku Israeli ikizuia.

Naibu Balozi wa Marekani Robert Wood alisema wazi siku ya Alhamisi kwamba utawala wa Biden ulipinga azimio jipya la bunge. Marekani ilikuwa miongoni mwa nchi tisa zilizopiga kura dhidi yake, pamoja na Israeli.

Chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa, wale wanaotarajiwa kuwa wanachama wa Umoja wa Mataifa ni lazima wawe “wapenda amani,” na Baraza la Usalama lazima lipendekeze kuandikishwa kwao kwenye Baraza Kuu kwa idhini ya mwisho. Palestina ilipata hadhi ya uangalizi na sio mwanachama wa umoja huo mnamo mwaka 2012.

"Tumekuwa wazi sana tangu mwanzo kuna mchakato wa kupata uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa, na juhudi hizi za baadhi ya nchi za Kiarabu na Wapalestina ni kujaribu kuzunguka hilo," Wood alisema Alhamisi.

"Tumesema tangu mwanzo njia bora ya kuhakikisha uanachama kamili wa Palestina katika Umoja wa Mataifa ni kufanya hivyo kupitia mazungumzo na Israeli. Huo unabaki kuwa msimamo wetu.”

Mashambulizi ya Israeli dhidi ya Wapalestina katika eneo la Gaza, yameingia siku ya 217, huku yakiua watu 34,943, asilimia 70 wakiwa wanawake na watoto wadogo, na kujeruhi wengine zaidi ya 78,572.

Miezi saba ya vita vya Israel, maeneo makubwa ya Gaza yamegeuka kuwa magofu, na kuwafanya asilimia 85 ya wakazi wa eneo hilo kuwa wakimbizi wa ndani huku kukiwa na kizuizi katika upatikanaji wa chakula, maji safi na dawa, kulingana na Umoja wa Mataifa.

Israeli inashutumiwa kwa mauaji ya halaiki katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki. Uamuzi wa muda wa mwezi Januari ulisema "inawezekana" kwamba Israeli inafanya mauaji ya halaiki huko Gaza na kuiamuru Tel Aviv kusitisha vitendo hivyo na kuchukua hatua za kuhakikisha kwamba msaada wa kibinadamu unatolewa kwa raia huko Gaza.

TRT Afrika