Uturuki imeonesha nia ya kuzungumza ukweli na kulinda nia thabiti ya watu wa Palestina, licha ya tuhuma zisizo na misingi./Picha: TRT World  

Serikali ya Uturuki imelaani chapisho la hivi karibuni lililowekwa kwenye mtandao wa kijamii la Waziri wa Mambo ya Nje wa Israeli Israel Katz, huku likiliita kuwa ni la uongo lenye kumlenga Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na Uturuki.

Katika taarifa rasmi iliyotolewa siku ya Jumamosi, mamlaka za Uturuki zimesema kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Israeli Israel Katz haaminiki, hata na serikali ya Netanyahu, ambayo inatekeleza uhalifu wa mauaji ya kimbari, ikiacha doa la kihistoria.

Kulingana na taarifa hiyo, Katz anajaribu kutafuta umuhimu kwa kuvuta hisia za watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini Uturuki katika jitihada za kupata nafasi yake ndani ya kile ilichokitaja kama "mtandao wa mauaji ya kimbari."

Uturuki imeonesha nia ya kuzungumza ukweli na kulinda nia thabiti ya watu wa Palestina, licha ya tuhuma zisizo na misingi.

Serikali ya Uturuki imesisitiza kuwa itaendelea kusimama kidete kuunga mkono haki na uadilifu wa Wapalestina.

TRT Afrika