Tangu vita vya Israel dhidi ya Gaza iliyozingirwa mnamo Oktoba 7 na muda mrefu kabla, Uturuki imekuwa bila kutetereka katika uungaji mkono wake kwa Palestina. / Picha: Jalada la AA

Uturuki imekanusha madai ya ushirikiano na Israel, hususan ushirikiano wa kiulinzi, akisema nchi hiyo haitafanya jambo lolote litakalowadhuru Wapalestina na malengo yao.

"Haiwezekani kwa Jamhuri ya Uturuki, ambayo siku zote imekuwa ikiiunga mkono Palestina, kufanya au kujihusisha na shughuli zozote ambazo zinaweza kuwadhuru Wapalestina," Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo ilisema Jumanne.

Wizara hiyo ilisema haina shughuli zozote na Israel, "ikiwa ni pamoja na mafunzo ya kijeshi, mazoezi na ushirikiano wa sekta ya ulinzi."

Kauli hiyo imekuja baada ya madai ya uwongo ya baadhi ya vyombo vya habari kuwa Uturuki inaendelea kusafirisha baruti, silaha na risasi kwa Israel.

Kando, Kituo cha Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki cha Kukabiliana na Upotoshaji pia kilikataa ripoti hizo baada ya kukagua machapisho kadhaa ya mitandao ya kijamii.

"Bidhaa katika sura ya 93 ya orodha inayodaiwa ya mauzo ya nje sio silaha za kivita na risasi lakini vipuri vya bunduki na vifaa vya uvuvi vinavyotumika kwa madhumuni ya kibinafsi kama vile michezo na uwindaji," ilisema kwenye X.

Kulingana na data kutoka Taasisi ya Takwimu ya Uturuki [TURKSTAT], hakujakuwa na mauzo ya bunduki kwa madhumuni ya michezo na uwindaji tangu Mei 2023, ambayo tayari ilikuwa na takwimu za chini, iliongeza.

"Bidhaa zilizosafirishwa nje ya nchi chini ya kichwa cha 'Baruti na vilipuzi, bidhaa za pyrotechnic, viberiti, aloi za pyrophoric, maandalizi yanayoweza kuwaka' katika sura ya 36 ya orodha ya mauzo ya nje yalikuwa 'mafuta ya gel na kioevu nyepesi.'

"Imebainishwa kuwa juhudi zilifanywa kuhadaa umma kuhusu bidhaa zilizojumuishwa katika vichwa vya sura ya Ushuru wa Forodha na kusafirishwa na makampuni ya kibinafsi," iliongeza.

Tangu vita vya Israel dhidi ya Gaza iliyozingirwa mnamo Oktoba 7 na muda mrefu kabla, Uturuki imekuwa bila kutetereka katika uungaji mkono wake kwa Palestina.

Mauaji ya kimbari ya Israel huko Gaza

Rais wa nchi hiyo Recep Tayyip Erdogan amesema, kuhamasisha uelewa wa "unyama" unaofanywa dhidi ya watu wa Gaza na kuzuia taarifa potofu za Israel ni miongoni mwa majukumu makuu ya Uturuki.

Israel pia imekuwa ikitumia fursa ya ushawishi wake juu ya mashirika ya vyombo vya habari vya kimataifa, wakati huo huo ikiharakisha juhudi zake za kutoa taarifa potofu, Erdogan alisema hivi karibuni.

Israel imeua watu wasiopungua 32,414 na kujeruhi 74,787 katika eneo lililozingirwa tangu shambulio l aHamas la Oktoba 7.

Hamas inasema jibu lake, ambalo baadhi ya wataalam wanalinganisha na uasi wa Wayahudi katika geto la Warsaw mwaka 1943, lilikuja kujibu mashambulizi ya mara kwa mara ya Israel dhidi ya Msikiti wa Al-Aqsa, ghasia za walowezi katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu na kurudisha swali la Palestina mezani."

Katika shambulio la kushangaza, watu wenye silaha wa Hamas waliingia katika maeneo mengi kama 22 nje ya Gaza, ikiwa ni pamoja na miji na jumuiya nyinginezo hadi kilomita 24 kutoka kwenye uzio wa Gaza.

Katika baadhi ya maeneo wanasemekana kuwafyatulia risasi wanajeshi wengi huku jeshi la Israel likihangaika kujibu. Na waliporudi Gaza, walichukua pia mateka wapatao 240, kutia ndani wanajeshi wa Israeli na raia.

Makumi ya mateka hao baadaye walibadilishwa na Wapalestina waliokuwa wamefungwa katika magereza ya Israel.

Tangu wakati huo, Israel imeua na kulemaza makumi ya maelfu na imesukuma asilimia 85 ya wakazi wa Gaza kama wakimbizi wa ndani kutokana na uhaba mkubwa wa chakula, maji safi na dawa, huku asilimia 60 ya miundombinu ya eneo hilo ikibomolewa au kuharibiwa, kulingana na UN.

Israel inashutumiwa kwa mauaji ya halaiki katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ambayo mwezi Januari ilitoa uamuzi wa muda ulioiamuru Tel Aviv kusitisha vitendo vya mauaji ya halaiki na kuchukua hatua za kuhakikisha kwamba msaada wa kibinadamu unatolewa kwa raia huko Gaza.

Siku ya Jumatatu, mtaalam mkuu wa haki za Umoja wa Mataifa alisema kulikuwa na "misingi ya busara" ya kuamua kwamba Israel imefanya vitendo kadhaa vya "mauaji ya halaiki" katika vita vyake huko Gaza, pia kuibua "usafishaji wa kikabila".

Francesca Albanese, mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki katika ardhi za Palestina amesema kuna dalili za wazi kuwa Israel imekiuka vitendo vitatu kati ya vitano vilivyoorodheshwa chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mauaji ya Kimbari.

TRT World