Gaidi Zeynep Secim anasemekana kufanya kazi kama mratibu wa mabomu katika eneo la Operesheni Claw-Lock, akilenga vikosi vya usalama. /Picha: Nyingine

Shirika la Kitaifa la Ujasusi la Uturuki (MIT) limemtambua gaidi aliyekatwa makali hivi majuzi kama Zeynep Sevim, aliyepewa jina la "Ruken Zilan," akiratibu ugavi wa zana za kundi la kigaidi la PKK.

Habari zilizopatikana kutoka kwa vyanzo vya usalama siku ya Jumatatu zinafichua kwamba gaidi huyo, ambaye 'alikatwa makali' huko Duhok, alikuwa akipanga mipango ya kukidhi mahitaji ya risasi ya wanachama wa PKK wanaopanga vitendo vya kigaidi dhidi ya vikosi vya usalama vya Uturuki.

Alijiunga na kada ya vijijini ya PKK/KCK mwaka wa 2014, ushiriki wa Sevim ulijumuisha shughuli katika maeneo ya Metina, Gara, na Avasin kaskazini mwa Iraq.

Zaidi ya hayo, anasemekana kufanya kazi kama mratibu wa silaha katika eneo la Operesheni Claw-Lock, akilenga vikosi vya usalama.

Dada yake Zeynep Sevim, anayejulikana kwa jina la "Zilan Ruken", Fatma Sevim, pia alikatwa makali na vikosi vya usalama katika operesheni iliyofanywa katika wilaya ya Ovacık ya Tunceli mnamo 2012.

Mamlaka ya Uturuki hutumia neno "kumkata makali " kumaanisha magaidi wanaohusika walijisalimisha au waliuawa au kukamatwa.

Uturuki ilizindua Operesheni Claw-Lock mwaka jana mwezi Aprili ili kulenga maficho ya kundi la kigaidi la PKK katika maeneo ya Metina, Zap, na Avasin-Basyan kaskazini mwa Iraq, yaliyo karibu na mpaka wa Uturuki.

Katika kampeni yake ya zaidi ya miaka 35 ya ugaidi dhidi ya Uturuki, PKK - iliyoorodheshwa kama shirika la kigaidi na Uturuki, Marekani, na EU - imehusika na vifo vya zaidi ya watu 40,000, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto wachanga.

TRT World