Rais wa Uturuki Erdogan atia saini itifaki ya Sweden ya kujiunga na NATO, atuma bungeni

Rais wa Uturuki Erdogan atia saini itifaki ya Sweden ya kujiunga na NATO, atuma bungeni

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan anasisitiza kuwa uwezekano wa Sweden kujiunga na NATO ni kwa uamuzi wa bunge la Uturuki
Hapo awali Uturuki iliidhinisha uanachama wa Finland katika NATO lakini ilikuwa imesema inasubiri Uswidi kutii mkataba wa pande tatu uliotiwa saini Juni 2022. / Picha: Kumbukumbu ya AA / Photo: AA Archive

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan Jumatatu alitia saini itifaki ya kujiunga na NATO ya Sweden na kuiwasilisha bungeni, kulingana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki.

Waziri Mkuu wa Sweden alikaribisha tangazo la Uturuki.

"Taratibu za bunge sasa zitaanza. Tunatazamia kuwa wanachama wa NATO," wizara ilisema kwenye X.

Finland na Uswidi zilituma maombi ya uwanachama wa NATO mara baada ya Urusi kuanzisha mashambulizi yake dhidi ya Ukraine mnamo Februari 2022.

Hapo awali Uturuki iliidhinisha uanachama wa Finland katika NATO lakini ilikuwa imesema inasubiri Uswidi kutii mkataba wa pande tatu uliotiwa saini Juni 2022 mjini Madrid ili kushughulikia masuala ya usalama ya Ankara.

Wanachama wote wa NATO - ikiwa ni pamoja na Uturuki, mwanachama wa zaidi ya miaka 70 - lazima waidhinishe wanachama wowote wapya wa muungano.

TRT World