Magaidi walifyatua risasi katika maeneo ya operesheni, ilisema Wizara ya Ulinzi. / Picha: Jalada la AA

Vikosi vya usalama vya Uturuki "vimewakata makali " magaidi wanne wa PKK/YPG waliofyatua risasi katika maeneo ya operesheni kaskazini mwa Syria, Wizara ya Ulinzi ya Kitaifa ilisema.

Katika taarifa yake kwenye X, mtandao wa kijamii uliokuwa zamani Twitter, wizara hiyo ilisema Jumanne kwamba Uturuki "inaendelea kuwadhibiti magaidi wanaotaka kuvuruga amani na usalama wa watu nchini Syria."

"Vikosi vya kishujaa vya jeshi la Uturuki vimewaangamiza magaidi 4 wa PKK/YPG ambao walifyatua risasi katika maeneo ya 'Olive Branch' na 'Peace Spring," iliongeza.

Katika kampeni yake ya zaidi ya miaka 35 ya ugaidi dhidi ya Uturuki, PKK - iliyoorodheshwa kama shirika la kigaidi na Uturuki, Marekani, na EU - imehusika na vifo vya zaidi ya watu 40,000, ikiwa ni pamoja na wanawake, watoto na watoto wachanga.

YPG ni kitengo chake upande wa Syria.

Tangu 2016, Ankara imezindua oparesheni tatu zenye mafanikio za kupambana na ugaidi katika mpaka wake kaskazini mwa Syria ili kuzuia uundaji wa ukanda wa ugaidi na kuwezesha makazi ya amani. - Euphrates Shield (2016), Olive Branch (2018) na Peace Spring (2019).

TRT World