Majeshi ya anga ya Uturuki kushiriki katika mazoezi ya pamoja ya 'Tiger Meet' 2024 nchini Ujerumani

Majeshi ya anga ya Uturuki kushiriki katika mazoezi ya pamoja ya 'Tiger Meet' 2024 nchini Ujerumani

Mchakato huo huwa ni wa muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa nchi wanachama wa NATO na kuonesha nguvu zao katika kulinda anga.
Ndege ya kijeshi ya F16 yenye muonekano wa Simbamarara ikiwa kwenye mazoezi ya 62 ya NATO Tiger/ Picha: AA  

Majeshi ya anga ya Uturuki yatashiriki katika zoezi la pamoja la NATO Tiger Meet 2024, ikitumia ndege zake tatu za kivita aina ya F-16.

Zoezi hilo litahusisha ndege za kivita zaidi ya 50 na washiriki 1,100 kutoka nchi 13 wanachama wa NATO, kulingana na taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya Jeshi la Anga la Ujerumani.

Jeshi la Anga la Ujerumani ndiye mwenyeji wa zoezi hilo kwa mwaka huu , ambalo pia limeandaliwa kwa miaka 63 na umoja huo wenye kumtumia Simbamarara kama nembo yake.

Zoezi hilo litafanyika katika kambi ya Schleswig/Jagel iliyoko kaskazini mwa Ujerumani, kuanzia Juni 3 hadi 14.

Kuimarisha ushirikiano

Mchakato huo huwa ni wa muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa nchi wanachama wa NATO na kuonesha nguvu zao katika kulinda anga.

Kati ya Juni 7 na 10, Jeshi hilo la anga litaruhusu wapiga picha kuingia eneo la kufanyia zoezi hilo.

Wapiga picha hao watapata fursa ya kupata picha za ndege tofauti zikiwemo Tornado, Eu rofighter, Griepen, F-16 na Rafale aircraft.

Ndege za bESİFDES, Heron TP ambayo haina rubani zitashiriki zoezi hilo.

TRT Afrika