Kampuni ya Uturuki ya kutengeza ndege zisizo na rubani yatunukiwa heshima ya kitaifa na Mali

Kampuni ya Uturuki ya kutengeza ndege zisizo na rubani yatunukiwa heshima ya kitaifa na Mali

Ujumbe wa Baykar ulikutana na rais wa mpito wa Mali Kanali Assimi Goita
Heshima hizo ni mapambo ya juu zaidi nchini na zilitolewa katika ikulu ya rais katika hafla / Picha:Others 

Viongozi wa kampuni ya kutengeneza ndege zisizo na rubani za Uturuki, Baykar Technologies wametunukiwa heshima ya kitaifa nchini Mali kwa mchango na huduma kwa nchi hiyo ya Afrika Magharibi.

Ujumbe huo wa watu wanne, ukiongozwa na mwenyekiti wa bodi Selcuk Bayraktar na mtendaji mkuu Haluk Bayraktar, walipokea heshima hizo Jumatano.

Heshima hizo ni mapambo ya juu zaidi nchini na iliyotolewa katika ikulu ya rais katika hafla iliyoshuhudiwa na Waziri wa Ulinzi wa Mali Kanali Sadio Camara.

Ujumbe wa Baykar pia ulikutana na rais wa mpito wa Mali Kanali Assimi Goita.

"Tuliheshimiwa kwa kuonekana kuwa tunastahili ushirikiano huu wa maana ili kuimarisha urafiki na ushirikiano kati ya Uturuki na Mali," Haluk Bayraktar alisema katika akaunti ya X, iliyoitwa zamani Twitter.

Tuzo ya Kitaifa ya Mali imetunukiwa wakuu wa nchi za kigeni kama ishara ya urafiki, pamoja na wale ambao wamechangia kwa maendeleo ya nchi hiyo.

Bayraktar ina maana sawa na uwezo wa kijeshi wa Uturuki kote ulimwenguni/Picha: Getty Images

Mwaka jana, Mali na Uturuki zilitia saini makubaliano ya ushirikiano katika nyanja ya ulinzi na usalama.

Bayraktar inaashiria nguvu ya kijeshi ya Uturuki kote ulimwenguni, huku mauzo yake ya nje yakifikia zaidi ya 80% ya mapato yake.

Ilipata umakini wa kimataifa kwa mafanikio yake katika uzoefu wa kutumika nchini Libya na hivi karibuni Ukraine.

Heshima hizo ni mapambo ya juu zaidi nchini na zilitolewa katika ikulu ya rais Picha: Mali

Mnamo Aprili, afisa mkuu mtendaji wa kampuni ya kutengeneza ndege zisizo na rubani za Uturuki Baykar alitunukiwa nishani ya serikali katika nchi jirani ya Burkina Faso, ambapo magari ya angani ya kampuni ya Bayraktar TB2 (UAVs) yamesafirishwa.

Haluk Bayraktar alipokea medali ya 'Ordre de L'etalon Officier', heshima kuu ya kitaifa ya nchi hiyo, kwa amri ya rais wa Burkina Faso Ibrahim Traore kwa mchango wake bora na wa kipekee katika shughuli za amani, usalama na kupambana na ugaidi za taifa hilo la Afrika Magharibi.

Uturuki pia imeuza ndege zisizo na rubani kwa nchi zingine tatu za Kiafrika: Morocco, Tunisia na Ethiopia.

Na Niger imeonyesha nia ya kununua ndege zisizo na rubani za TB2 Bayraktar.

TRT Afrika