| Swahili
UTURUKI
2 DK KUSOMA
Hamas yakabidhi miili ya mateka kwa Msalaba Mwekundu
Makubaliano ya kusitisha mapigano Gaza, yameingia siku yake ya 33. Mashambulizi ya Israeli Gaza yanaripotiwa kuuwa zaidi ya Wapalestina 48,297, takwimu ambazo baada ya kupitiwa upya zinakaribia 62,000.
Hamas yakabidhi miili ya mateka kwa Msalaba Mwekundu
Zoezi la kurudisha miili hiyo limefanyika kusini mwa Gaza katika mji wa Khan Younis. / Picha: AFP / AFP
20 Februari 2025

Hamas imekabidhi kwa Shirika la Msalaba Mwekundu miili ya mateka wanne waliouliwa katika mashambulizi ya Israeli Gaza, kwa mujibu wa TRT World.

Shirika la Msalaba Mwekundu limeelekea sehemu ya Gaza kupokea miili ya mateka wanne wa Israeli ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya usitishaji wa mapigano, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Israeli.

Zoezi la kupeana kwa miili hiyo limefanyika kusini mwa Gaza katika mji wa Khan Younis.

Kabla ya kuwasilishwa kwa miili hiyo, mamia ya watu walikusanyika katika eneo lililotumika kama makaburi. Kumewekwa uzio ili kuzuia watu kufika katika eneo lililotengwa kufanyika zoezi la kupeana miili hiyo.

Hamas imeonyesha majeneza manne yaliyowekwa katika jukwaa Gaza.

Hamas imesema itapeana miili ya Shiri Bibas, Kfir, Ariel, na Oded Lifshitz.

CHANZO:TRT World