Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier wametoa rai ya kuongezeka kwa juhudi za kimataifa za kusitisha mapigano huko Gaza na uwepo wa dola mbili katika mgogoro baina ya Israeli na Palestina.
Wakizungumza katika mkutano na wanahabari jijini Ankara siku Jumatano, viongozi hao waliweka msisitizo kwenye nafasi ya diplomasia na kuonya dhidi ya hatua zinazolenga kudidimiza sheria za kimataifa.
Erdogan alisisitiza umuhimu wa jumuiya ya kimataifa kufuatilia kwa karibu na kusitisha mapigano hayo ili kufikia suluhisho la kidiplomasia katika mgogoro huo.
TRT Afrika