Droo ya Afcon itafanyika Abidjan tarehe 12 Oktoba 2023 kabla ya kombe hilo kuanzika Januari mwaka ujao. Picha: CAF

Timu 16 bora Afrika kulingana na orodha ya FIFA, zimefuzu kwenye fainali hizo huku ikitarajiwa kuleta ushindani mkali kwenye ngarambe za mwaka huu.

Cameroon na Namibia zilijiunga na mwenyeji wa mashindano hayo, Cote D'ivoire na timu zingine 22 zilizohitimu kwenye mashindano hayo yatakayoanza Januari mwaka ujao.

Afrika Magharibi inawakilishwa na mabingwa mbalimbali wakiwemo wenyeji Cote D'ivoire, mabingwa tetezi Senegal, Mabingwa mara nne Ghana na washindi wa 2013 Nigeria, pamoja na Burkina Faso, Guinea Bissau, Guinea, Mali, Mauritania na Gambia ambao walifunga safari ya kufuzu kwa vishindo.

Afrika Kaskazini inawakilishwa na Morocco iliyofika nusu fainali ya kombe la dunia, Tunisia, Algeria, Misri wanaotabiriwa kuwa miongoni mwa mabingwa wa tarajiwa wa kombe hilo.

Misri inatafuta taji lake la nane baada ya kutinga fainali mara mbili kati ya mashindano matatu zilizopita mnamo 2017 na katika toleo la 2021. Aidha, washindi wa mwaka wa 1990 na 2019, Algeria inarudi kwenda kwa jina la tatu.

Afrika Mashariki itakuwa na mwakilishi mmoja pekee baada ya Tanzania kurejea fainali hizo tangu 2019, kwa kuipiku Uganda.

Cote d’Ivoire (wenyeji), Algeria, Angola, Burkina Faso, Cameroon, Cape Verde, DR Congo, Misri, Equatorial Guinea, Gambia, Ghana, Guinea, Guinea-Bissau, Mali, Mauritania, Morocco, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Senegal, Afrika Kusini, Tanzania, Tunisia na Zambia

Dimba hilo, ambalo ni mojawapo ya matukio makubwa ya michezo duniani, litang'oa nanga Abidjan, Cote D'ivoire, tarehe 13 januari 2023.

TRT Afrika