| Swahili
AFRIKA
1 DK KUSOMA
Vyama vya siasa Tanzania vyatakiwa kuchagua viongozi wao
Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania inasema kuwa muda wa uongozi kwenye baadhi ya vyama vingi umefikia kikomo, bila vyama hivyo kuchangua viongozi.
Vyama vya siasa Tanzania vyatakiwa kuchagua viongozi wao
Baadhi ya watanzania wakishirika zoezi la upigaji kura katika moja ya uchaguzi nchini Tanzania./Picha: Wengine / Others
18 Januari 2024

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania imevitaka vyama ambavyo havijachaguza viongozi wake kufanya hivyo, kabla muda kuisha.

Hii ni kufuatia ofisi hiyo kubaini uwepo wa idadi kubwa wa vyama vya siasa ambavyo muda wa viongozi wake kukaa madarakani umefikia kikomo, kufikia mwaka huu.

"Kwa mujibu wa sheria, kila chama cha siasa kinapaswa kufanya uchaguzi wa kidemokrasia wa viongozi wake kwa vipindi ambavyo vimewekwa katika Katiba yake...vilevile uchaguzi wa viongozi wa chama cha siasa unapaswa kufanyika sio zaidi ya miaka mitano tangu uchaguzi uliopita kufanyika," inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Tanzania ina jumla ya vyama vya siasa 19, vyenye usajili kamili kutoka ofisi hiyo.

CHANZO:TRT Afrika