Vituo vya kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa rais na wabunge vya funguliwa Uturuki

Vituo vya kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa rais na wabunge vya funguliwa Uturuki

Wapiga kura kutoka kote nchini wataelekea katika vituo vyao vya kupigia kura ili kutekeleza haki yao ya kidemokrasia.
Vituo vya kupigia kura vitafungwa saa kumi na moja jioni kwa saa za hapa nchini na matokeo ya kwanza yanatarajiwa kuanza kutolewa muda mfupi baada ya hapo. / Picha: AA

Vituo vya kupiga kura vimefunguliwa kote Uturuki mapema siku ya Jumapili asubuhi kwa uchaguzi wa rais na wabunge nchini humo.

Rais wa sasa Recep Tayyip Erdogan anawania muhula wake wa mwisho madarakani, wakati wagombea wa upinzani ni Kemal Kilicdaroglu wa Muungano wa Nation na Sinan Ogan wa Ata Alliance.

Bodi ya Juu ya Uchaguzi (YSK) ilitangaza mapema kwamba zaidi ya raia milioni 64 wanastahili kupiga kura katika uchaguzi wa Mei 14, ikiwa ni pamoja na wapiga kura zaidi ya milioni 3 nje ya nchi.

Upigaji kura utafungwa saa kumi na moja jioni saa za ndani, na matokeo ya kwanza yanatarajiwa kuanza kuja muda mfupi baada ya hapo.

Wapiga kura nchini Uturuki wanahitaji kuonyesha vitambulisho vyao au hati nyingine rasmi za utambulisho katika vituo vya kupigia kura.

Kisha, kila mpiga kura hupewa karatasi mbili tofauti za kupigia kura, moja kwa ajili ya uchaguzi wa urais na moja kwa ajili ya uchaguzi wa ubunge. Wapiga kura huweka alama kwenye karatasi zao za kupigia kura na kisha kuziweka kwenye bahasha.

Kulingana na shirika la uchaguzi la Uturuki, wapiga kura hawaruhusiwi kupiga picha au video zozote ndani ya kibanda cha kupigia kura, na wanaacha simu zao nje.

Baada ya kumalizika kwa upigaji kura, kura zilizopigwa kwa wagombea urais huhesabiwa kwanza mbele ya kamati ya upigaji kura ambayo inajumuisha wajumbe wa baraza la uchaguzi la Uturuki na vyama vya siasa pamoja na raia wanaotaka kubaki humo.

Wananchi wote wanaweza kupiga kura

Baraza la uchaguzi la Uturuki limechukua hatua kurahisisha upigaji kura kwa raia wote, bila kujali uwezo wao wa kimaumbile.

Kwa wale ambao hawawezi kuondoka kwenye nyumba zao au vitanda vya hospitali, kuna masanduku ya kura yanapitishwa. Sanduku hizi huletwa kwenye eneo la mpiga kura, ili waweze kupiga kura yao kwa faragha.

Vinginevyo, wapiga kura wanaweza kusafirishwa hadi kwenye masanduku ya kura kwa usaidizi wa ambulensi bila malipo. Baraza la uchaguzi pia limetoa vielelezo maalum vya kupiga kura kwa wananchi wenye ulemavu wa macho. Vielelezo hivi vina maandishi makubwa na Braille, ili wananchi wenye matatizo ya kuona waweze kupiga kura kwa kujitegemea na kwa siri.

Mipango hii inahakikisha kwamba wananchi wote wanaweza kushiriki katika mchakato wa kidemokrasia kwa heshima.

Kura za waliopo ughaibuni zimeletwa Uturuki kwa njia ya ndege na zitahesabiwa kwa wakati mmoja na kura zilizopigwa Uturuki. Upigaji kura kwenye lango la forodha ulianza Aprili 27 na kumalizika Mei 9.

Katika uchaguzi mkuu, chama cha siasa kinapaswa kupata asilimia 10 ya kura nchi nzima ili mgombeaji wake yeyote apate nafasi ya ubunge. Muungano pekee ndio unahitaji kupitisha kiwango cha asilimia 10 ili vyama viweze kudai viti bungeni.

Katika siku ya uchaguzi mashirika ya vyombo vya habari hayaruhusiwi kutangaza matangazo yoyote ya kisiasa, ubashiri au maoni kuhusu uchaguzi hadi 06.00 p.m. (1500GMT). Kati ya 06.00 PM. (1500GMT) na 09.00 P.M. (1800GMT), vyombo vya habari vitaweza tu kuchapisha matangazo rasmi kuhusu uchaguzi yanayotolewa na Baraza Kuu la Uchaguzi.

Uzaji wa vileo umepigwa marufuku kutoka saa 12.00 asubuhi (0300GMT) hadi sita usiku, (2100GMT), lakini pia unywaji wa vileo pia umepigwa marufuku katika maeneo ya umma.

TRT World