Polisi wa kitaifa wa Liberia wametuma maafisa wa ziada kusaidia katika msako wa wafungwa waliotoroka. / Picha: AA / Picha: mitandao ya kijamii

Makumi ya wafungwa walitoroka kutoka kwenye gereza lenye ulinzi mkali nje ya mji mkuu wa Liberia mwishoni mwa juma, mamlaka ilisema Jumatatu.

Wafungwa 47 waliweza kutoroka kwa sababu ya ukiukaji wa mfumo wa usalama wa magereza, Wizara ya Sheria ilisema katika taarifa.

Gereza hilo liko Kakata, mji ulio umbali wa kilomita 55 (maili 34) kaskazini mashariki mwa mji mkuu, Monrovia.

Wizara hiyo ilisema "ina wasiwasi mkubwa juu ya tukio hili na inachukua hatua zote muhimu ili kuhakikisha kuwa wafungwa waliotoroka wanakamatwa tena."

Polisi wa ziada wanajiunga na utafutaji

Polisi wa kitaifa pia wametuma maafisa wa ziada kusaidia katika msako wa waliotoroka, wizara ilisema.

Magereza nchini Libeŕia mara nyingi yana msongamano mkubwa, na wafungwa wanakosa kupata chakula cha kutosha na huduma za kimsingi za kimatibabu.

Mwaka jana, gereza moja huko Monrovia lilikosa chakula, na magereza mengine mawili yaliacha kuchukua wafungwa kwa muda mfupi kwa sababu ya uhaba wa chakula.

Idadi kubwa ya wafungwa pia wanazuiliwa bila kesi. Mnamo Novemba 2022, ripoti ya Umoja wa Mataifa iligundua kuwa 73% ya idadi ya wafungwa nchini kote walikuwa wafungwa kabla ya kesi.

TRT Afrika