Misri: Watu 37 waliokolewa baada ya boti ya watalii kuzama katika Bahari Nyekundu

Misri: Watu 37 waliokolewa baada ya boti ya watalii kuzama katika Bahari Nyekundu

Boti hiyo ilikuwa imebeba wageni 26 na Wamisri 11
Bahari Nyekundu / Photo: AFP

Takriban watu 37 waliokolewa baada ya mashua iliyokuwa imebeba watalii kuzama kaskazini mwa Misri katika Bahari Nyekundu, jeshi la Misri lilisema Alhamisi.

"Jeshi la Wanamaji la Misri lilifanikiwa kuwaokoa watu 37 wa mataifa tofauti waliokuwa kwenye boti ya watalii baada ya kupinduka," msemaji wa jeshi la Misri Gharib Abdel Hafez alisema katika taarifa.

"Boti hiyo ilikuwa na Waingereza 14, Wajerumani watatu, Wabelgiji wanne, Wahispania watatu, raia wa ireland na Mswizi, pamoja na Wamisri 11 miongoni mwa wafanyakazi na wapiga mbizi," aliongeza.

Alisema abiria waliookolewa walipata huduma ya matibabu baada ya kuwasili kwenye gati katika Kituo cha Wanamaji cha Bahari Nyekundu.

Abdel Hafez hakutoa maelezo zaidi juu ya hali ya afya ya abiria.

TRT Afrika na mashirika ya habari