Mhubiri Mackenzie wa Kenya katika kesi ya 'kipekee' ya kuua bila kukusudia

Mhubiri Mackenzie wa Kenya katika kesi ya 'kipekee' ya kuua bila kukusudia

Mhubiri wa Kenya Paul Mackenzie ameshtakiwa kwa mauaji ya mamia ya wafuasi wake mwaka jana
Mackenzie na washtakiwa wengine 29 walikanusha mashtaka walipokabiliana na Hakimu Mkuu, Jaji Mugure Thande. Picha: Reuters

Kiongozi wa kikundi cha njaa cha Kenya alianza kushtakiwa kwa mauaji ya bila kukusudia siku ya Jumatatu akihusishwa na vifo vya zaidi ya wafuasi wake 400 katika moja ya majanga mabaya na makubwa zaidi yanayohusiana na kikundi cha imani potofu duniani.

Mchungaji anayejiita Paul Nthenge Mackenzie, na washukiwa wengine kadhaa walikana mashtaka mnamo Januari ya makosa mengi ya mauaji ya bila kukusudia, moja ya kesi kadhaa dhidi yao kuhusiana na kile kinachojulikana kama "Mauaji ya Msitu wa Shakahola".

Mackenzie alikuwa mahakamani mjini Mombasa, pamoja na washukiwa wengine 93, waendesha mashtaka na maafisa wa mahakama walisema.

"Hakujawahi kuwa na kesi ya mauaji ya bila kukusudia kama hii nchini Kenya," mwendesha mashtaka Alexander Jami Yamina aliambia AFP, akiongeza kwamba watashtakiwa chini ya sheria ya Kenya inayoshughulikia makubaliano ya kujiua.

Kesi ya 'Kipekee Sana'

"Hii itakuwa kesi ya kipekee sana ya mauaji bila kukusudia."

Inadaiwa kuwa Mackenzie aliwahamasisha wafuasi wake kufa njaa ili "wakutane na Yesu" katika kesi iliyozua hofu nchini Kenya na kote duniani.

Alitiwa mbaroni mwezi Aprili mwaka jana baada ya miili kadhaa kugunduliwa kwa mara ya kwanza katika msitu wa Shakahola ulioko Malindi kando ya Bahari ya Hindi.

Waokoaji walitumia miezi kadhaa kutafuta katika vichaka na sasa wamegundua miili karibu 448 kutoka makaburi ya umati.

Watu walikufa kwa njaa

Matukio ya Janga la maafa Shakahola

Uchunguzi wa maiti ulionyesha kuwa wengi wa waathiriwa walikufa kwa njaa. Lakini wengine, wakiwemo watoto, inaonekana walinyongwa au kupigwa.

Nyaraka za mahakama za awali pia zilisema kuwa baadhi ya miili ilikuwa imeondolewa viungo.

Orodha ya mashtaka inataja washitakiwa 95 – wanaume 55 na wanawake 40 ikiwa ni pamoja na mke wa Mackenzie.

Lakini mwanamke mmoja aliyeshitakiwa alikufa akiwa chini ya ulinzi wa polisi kutokana na "matatizo yanayohusiana na ugonjwa wa muda mrefu na athari za kufunga," Yamina aliambia AFP, akiongeza kuwa alifariki "mwezi mmoja hivi uliopita."

AFP