Rais Ali Bongo, akipiga kura | Picha: Reuters

Kikundi cha maafisa wa kijeshi wa ngazi ya juu kimetangaza kupitia televisheni ya taifa nchini Gabon kusema wamelichukua madaraka kwa sababu uchaguzi uliofanyika mwishoni mwa wiki haukuwa na uaminifu.

Maafisa hao, waliotokea kwenye kituo cha habari cha Gabon 24 mapema siku ya Jumatano asubuhi, walisema wameufuta uchaguzi, kuvunja taasisi zote za serikali, na kufunga mipaka ya nchi.

Walidai wanawakilisha vikosi vyote vya usalama na ulinzi vya Gabon.

Tangazo hilo lilitolewa muda mfupi baada ya chombo cha uchaguzi cha serikali kutangaza kuwa Rais Ali Bongo Ondimba ameshinda mhula wa tatu madarakani katika uchaguzi wa Jumamosi.

"Kwa niaba ya watu wa Gabon... tumekujaamua kulinda amani kwa kumaliza utawala wa sasa," maafisa hao walisema.

Kituo cha Uchaguzi cha Gabon kilisema Bongo alipata asilimia 64.27 ya kura ikilinganishwa na asilimia 30.77 alizopata mpinzani wake mkuu Albert Ondo Ossa, baada ya mchakato kucheleweshwa.

TRT Afrika