G20: EU inaunga mkono wito wa kujumuisha AU kama mwanachama

G20: EU inaunga mkono wito wa kujumuisha AU kama mwanachama

Kwa sasa Afrika Kusini ndiyo pekee mwanachama wa G20 kutoka bara la Afrika.
India inatarajiwa kuongeza uwanachama wa kambi hiyo ili kujumuisha Umoja wa Afrika, / Picha: Reuters

Umoja wa Afrika iko tayari kujiunga kuwa mwanachama mpya zaidi wa G20, maafisa walisema Ijumaa, huku jitihada za umoja huo zikipata kuungwa mkono na wanachama waliokusanyika kwa ajili ya mkutano wao mkuu nchini India.

Mwenyeji wa G20 na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi ametoa wito kwa shirika hilo la mataifa ya Afrika kuwa mwanachama wa kudumu, akisema mataifa yanayoendelea yanahitaji sauti zaidi katika kufanya maamuzi duniani.

Pendekezo hilo limeungwa mkono na Washington na siku ya Ijumaa Umoja wa Ulaya ulisema pia utaunga mkono hatua hiyo.

"Ninatazamia kukaribisha AU kama mwanachama wa kudumu wa G20," rais wa Baraza la Ulaya Charles Michel aliwaambia waandishi wa habari mjini New Delhi, ambako mkutano wa kilele wa siku mbili wa G20 unaanza Jumamosi.

Pato la Dunia

Kundi la nchi 20 zenye uchumi mkubwa kwa sasa lina nchi 19 na Umoja wa Ulaya, zinazounda takriban 85% ya Pato la dunia na theluthi mbili ya idadi ya watu duniani.

Lakini Afrika Kusini kwa sasa ndiyo pekee mwanachama wa G20 kutoka bara la Afrika.

AU yenye makao yake makuu ya Ethiopia iliundwa mwaka 2002 kufuatia kusambaratika kwa Umoja wa Umoja wa Afrika.

Uamuzi unatarajiwa

Kwa ukamili wake ina wanachama 55, lakini mataifa sita yanayoongozwa na junta kwa sasa yamesimamishwa. Kwa pamoja ina Pato la $3 trilioni na jumla ya takriban watu bilioni 1.4.

Afisa mkuu wa huduma ya kigeni wa India Vinay Kwatra alisema alitarajia uamuzi kuhusu uanachama wa AU utafanywa katika mkutano huo Jumamosi asubuhi.

Hata hivyo, G20 imegawanyika sana katika masuala muhimu kuanzia vita vya Urusi nchini Ukraine hadi mabadiliko ya hali ya hewa, na bado kuna uwezekano wa mwanachama yeyote kupinga pendekezo hilo .

Azali Assoumani, rais wa visiwa vidogo vya Bahari ya Hindi vya Comoro na mkuu wa sasa wa Umoja wa Afrika, alitua New Delhi siku ya Ijumaa na kukaribishwa kwa zulia jekundu.

Imesubiriwa muda mrefu

Mwezi Desemba, Rais wa Marekani Joe Biden alisema alitaka AU "ijiunge na G20 kama mwanachama wa kudumu", akiongeza kuwa "imekuwa muda mrefu kufanyika hilo, lakini sasa muda umewadia".

Siku ya Jumanne, mshauri wa usalama wa kitaifa wa Biden alisisitiza msimamo huo wakati wa kujadili vipaumbele vya Marekani kwa mkutano wa kilele wa New Delhi.

"Pia tunatazamia kuukaribisha kwa moyo mkunjufu Umoja wa Afrika kama mwanachama wa kudumu wa G20 - mwanachama mpya kabisa wa kudumu. Tunaamini kuwa sauti ya Umoja wa Afrika itaifanya G20 kuwa na nguvu," Jake Sullivan alisema katika mkutano na White House.

TRT Afrika